AWADHI APIGA HAT TRICK,SIMBA IKIITWANGA MAFUNZO 3-0 NDANI YA AMAANA STADIUM


Simba imecheza mechi ya kirafiki na kufanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Mafunzo huku kiungo wake Awadhi Juma akionyesha uhai kwa kufunga mabao yote matatu, yaani hat trick.

Awadhi amefunga mabao hayo katika mechi hiyo ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, leo.

Simba imeweka kambi Zanzibar kujiandaa na mechi yake ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Azam FC, keshokutwa Jumapili.

Mechi hiyo ilianza taratibu huku Mafunzo wakiupoozesha mpira kabla ya kulazimishwa kuchangamka baada ya kuwaona Simba wakishambulia mfululizo.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment