Kocha wa timu ya taifa ya Ureno Fernando Santos leo
Jumatatu ya May 30 2016, amenukuliwa na vyombo vya habari hususani
dailymail akithibitisha kuwa katika mchezo wa kirafiki kati ya timu yake
dhidi ya timu ya Uingereza utakaochezwa June 2 2016 katika uwanja wa Wembley Cristiano Ronaldo na Pepe hawatocheza.
Fernando Santos
amesema hayo kutokana na nyota hao kuwa na uchovu, kwani toka wamalize
mchezo wa fainali ya Klabu Bingwa Ulaya kati ya klabu yao ya Real Madrid dhidi ya Atletico Madrid uliochezwa May 28 2016 Milan Italia, hawajapata muda wa kupumzika hivyo wanahitaji wiki moja ya kupumzika.

Ronaldo na Pepe
“Siwapumzishi
kwa sababu ya kukwepa majeruhi ila ni kwa ajili ya kuwaweka fiti tu,
nafikiri Cristiano Ronaldo atajiunga na timu Jumamosi akiwa na hali ya
kujiamini, ni mchezaji bora wa dunia na yeye ni muhimu kwa timu”

0 comments:
Post a Comment