FIFA YAMTANGAZA KATIBU MKUU WAKE MPYA, NI MWANAMAMA KUTOKA SENEGAL


Shirikisho la Soka la Kimataifa (Fifa), limemtangaza katibu wake mkuu mpya, safari hii akiwa ni mwanamama tena kwa mara ya kwanza.

Rais wa Fifa, Gianni Infantino, amemtangaza Fatma Samoura aria wa Senegal.
Fatma anakuwa mwanamke wa kwanza duniani kushika nafasi ya juu katika mchezo wa soka.

Mwanamama huyo anatarajia kuanza kazi yake rasmi mwezi ujao, na Infantino amesema hakukuwa na shinikizo wala ushawishi badala yake kazi nzuri ya Fatma.


Kwa sasa, Fatma ni mfanyakazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa (UN) akiwa nchini Nigeria.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment