
Jana Leicester, waliokuwa wakihitaji Pointi 3 tu kutwaa Ubingwa, walitoka Sare 1-1 na Manchester United huko Old Trafford.
Timu pekee iliyobaki ambayo inaweza kuwapiku Leicester Ubingwa ni Tottenham ambayo Leo inahitaji ushindi dhidi ya Chelsea ili kuweka hai matumaini yao.

Endapo Leo Spurs watatoka Sare au kufungwa basi Ubingwa ni wa Leicester waliobakisha Mechi mbili.
Ikiwa Spurs watashinda hii Leo basi Leicester, ambao wako chini ya Meneja kutoka Italy Claudio Ranieri aliewahi kuiongoza Chelsea, wanaweza kutwaa Ubingwa Nyumbani kwao King Power Stadium Jumamosi wakiifunga Everton.
Mechi hii ni ngumu kwa Spurs kwani mbali ya kuwa ni Dabi ya Jiji la London, Wachezaji wa Chelsea, kama vile Eden Hazard na Cesc Fabregas, wameapa ni bora Ubingwa uende kwa Leicester na si kwa Mahasimu wao Spurs.
LIGI KUU ENGLAND
Ratiba
**Saa za Bongo
Jumatatu Mei 2
2200 Chelsea v Tottenham
Jumamosi Mei 7
1445 Norwich v Man United
[Saa 11 Jioni]
Aston Villa v Newcastle
Bournemouth v West Brom
Crystal Palace v Stoke
Sunderland v Chelsea
West Ham v Swansea
1930 Leicester v Everton
Jumapili Mei 8
1530 Tottenham v Southampton
[Saa 12 Jioni]
Liverpool v Watford
Man City v Arsenal
Jumanne Mei 10
2145 West Ham v Man United
Jumatano Mei 11
[Saa 3 Dak 45 Usiku]
Norwich v Watford
Sunderland v Everton
2200 Liverpool v Chelsea
Jumapili Mei 15
**Mechi za Mwisho za Ligi, zote kuanza Saa 11 Jioni
Arsenal v Aston Villa
Chelsea v Leicester
Everton v Norwich
Man United v Bournemouth
Newcastle v Tottenham
Southampton v Crystal Palace
Stoke v West Ham
Swansea v Man City
Watford v Sunderland
West Brom v Liverpool

0 comments:
Post a Comment