Headlines za makocha wa soka kupoteza
ajira zao zinazidi kugonga vichwa vya habari kila kukicha duniani kote,
Alhamisi ya May 12 2016 jina la kocha Roberto Martinez limeingia kwenye list ya makocha waliofukuzwa Ligi Kuu Uingereza msimu huu wa 2015/2016.
Baada ya kupokea vipigo, klabu ya Everton imetangaza kumfukuza kazi kocha wake Roberto Martinez, Everton hivi karibuni kabla ya mchezo wa jana usiku kukubali kipigo cha goli 3-0 kutoka kwa Sunderland, katika michezo yake mitano iliyopita ilikuwa imefungwa mechi tatu, sare mechi moja na ushindi mechi moja.

Roberto Martinez
Kwa sasa Everton ambayo
imebakiza mechi moja ili kumaliza msimu wa Ligi Kuu Uingereza, ipo
nafasi ya 12 katika msimamo wa Ligi, imecheza mechi 37, ina point 44,
imefungwa mechi 13, imeshinda mechi 10 na kutoa sare mechi 14, hii ni
kwa mujibu wa Sky Sports na BBC.

0 comments:
Post a Comment