SASA KUBEBA TUZO YA BALLON D'OR, YAONEKANA NJIA NYEUPE KWA CRISTIAN RONALDO



Baada ya kuiwezesha Real Madrid kubeba ubingwa wa Ligi ya Mabingwa kwa mara ya 11, mshambuliaji Cristiano Ronaldo ndiye anapewa nafasi kubwa zaidi kubeba tuzo ya Ballon d'Or.

Ronado anapewa nafasi kutwaa tuzo hiyo ambayo tayari ameibeba mara tatu kwa kuwa mpinzani wake, Lionel Messi aliishia katikati baada ya Barcelona kuvuliwa ubingwa.

Raia huyo wa Ureno alifunga penalti ya mwisho wakati Madrid ilipoifunga Atletico Madrid kwa penalti 5-3 katika mechi ya fainali mjini Milan, Italia, wiki iliyopita.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment