Tangazo la ubaguzi wa rangi China lazua utata



Image captionTangazo China

Kampuni moja huko China imeomba msamaha kwa tangazo la sabuni ambalo limezua utata kwa madai ya ubaguzi wa rangi.
Kampuni hiyo ya Qiaobi , imesema imepinga na kushtumu ubaguzi wa rangi na kuomba radhi kwa tangazo hilo ambalo limezua utata.
Katika tangazo hilo,linamuonyesha mwanamume mweusi akiingiza kichwa chake kwenye mashine ya kufua na baadaye kujitoa akiwa na ngozi nyeupe ya raia wa ki-asia.

Image copyrightQIAOBI
Image captionTangazo China

Katika taarifa yao ya kuomba msamaha ,kampuni hiyo ya vipodozi ya Shanghai Leishang, imelaumu vyombo vya habari vya kimataifa kwa kulishtumu tangazo hilo.
Tangazo hilo lilitolewa mara ya kwanza mwezi Machi na kusimamishwa wiki hii kufuatia shinikizo kali.
Katika taarifa hiyo waliwaomba radhi Wafriaka wote na kusema ni matumaini yao kwamba watu na vyombo vya habari hawatazingatia tangazo hilo.

Image copyrightQIAOBI
Image captionTangazo China

Kampuni hiyo imesema imevifuta viunganishi vyote vya tangazo hilo na kuwataka watu kusitisha usambazaji wake kwenye mitandao.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment