Nahodha
wa timu ya taifa ya Kenya, Victor Wanyama anayekipiga Southampton ya
England amekisifia kikosi cha Taifa Stars kwa kuonyesha soka safi huku
akishangazwa kwamba hakukuwa na mchezaji hata mmoja wa kulipwa.
Stars ilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Kenya kwenye Uwanja wa Moi Kasarani jijini Nairobi, jana na kutoka sare ya bao 1-1.
“Unasema leo hamkuwa na professional pale uwanjani?” alionyesha kushangaa Wanyama.
“Basi
mna kikosi kizuri. Wengi ni vijana, wanaweza kama mkicheza kwa kutubana
kama mlivyobana hapa, Misri mnaifunga na hata hao Nigeria, si ajabu
nikasikia mnakwenda Afcon mwakani. Ninaitakia kila la khetri timu hii,
nawatakiwa kila la kheri Watanzania katika harakati zao.
"Sisi
mwaka huu tumepotea kabisa, hatuna matumaini tena, tunajipanga ndiyo
maana nimekuja kutetea taifa langu, hata kama tumekosa nafasi,” alisema
Wanyama anayekipiga Southampton ya England.
Katika
mchezo huo, Taifa Stars iliwakosa nyota wake Mbwana Samatta anayechezea
Genk ya Ubelgiji kwa kuwa alikuwa na mchezo muhimu wa kupa nafasi timu
yake ama icheze Ligi ya Uropa au ibaki nje katika michezo ya kimataifa
ngazi ya klabu Ulaya.
Shirikisho
la Soka Tanzania na Kocha Mkwasa walimruhusu kama ilivyo kwa Thomas
Ulimwengu anayekipiga TP Mazembe waliokuwa na mchezo mkali dhidi ya AS
Vita ambao wana utani na ushindani mkali wa soka huko Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo (DRC).



0 comments:
Post a Comment