Bekele aachwa nje ya kikosi cha Rio de Janeiro

Image copyrightREUTERS
Image captionKenenisa Bekele
Bingwa wa zamani wa mbio ndefu duniani Haile Gebreselassie ameshtumu shirikisho la riadha nchini Ethiopia kwa kumwacha bingwa mara tatu wa mashindano ya Olimpiki Kenenisa Bekele nje ya kikosi cha taifa hilo kinachoelekea katika michezo ya Olimpiki ya Rio de Jeneiro mnamo mwezi Agosti.
Haile aliambia BBC kwamba Bekele alifaa kuorodheshwa katika kikosi cha Marathon bila pingamizi yoyote kutokana na rekodi yake nzuri.
Shrikisho la riadha nchini Ethiopia linasema kuwa Kenenisa aliwachwa kwa kuwa hakuafikia mahitaji ya kikosi hicho.
Image captionGabresellassie
Kenenisa amekosoa uamuzi huo akisema haukuwa wa haki.
Bekele alikuwa wa tatu katika mashindano ya Lonmdon marathon mnamo mwezi Aprili,licha ya kutofanya mazoezi kamili na alishinda mbio za marathon za Great Manchester Run mwezi uliopita.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment