
Kama nimpenda michezo leo kuna mambo mawili unatakiwa kufahamu kutoka katika baraza la michezo la Taifa BMT, Baraza la michezo la Taifa leo May 31 2016 limetangaza rasmi kusimamisha shughuli za biashara za ngumi za ndani na nje zilizokuwa zikiratibiwa na PST hadi May 31 2020.
Serikali kupitia kwa kaimu katibu mkuu wa baraza hilo Kiganja wametangaza kufanya uamuzi huo leo May 31 2016 “PST wamesimamishwa kuratibu na kusimamia mchezo wa ngumi kuanzia leo May 31 2016 hadi May 31 2020, hao wamefungiwa lakini michezo ambayo tayari iliyokuwa imeratibiwa na PST itamaliziwa na BMT, kuhusu Yanga tulisikia kuna mtu TFF anakwamisha uchukuaji fomu ila hakuna kisingizo fomu zitolewe hadi weekend”

0 comments:
Post a Comment