
Nahodha wa
Manchester United Wayne Rooney, amekiri kuwa sasa anakabiliwa na
changamoto mpya katika Maisha yake ya Soka lakini amesisitiza bado
hajaishiwa na ustadi wa kucheza.
Rooney ambaye Jumatatu atatimiza
miaka 31, alitoa kauli hiyo alipoongea na Waandishi wa habari siku
chache baada ya Man United kutoka sare tasa 0-0 na Liverpool Jumatatu
iliyopita huko Anfield huku yeye akianzia Benchi.Rooney ameuelezea mchezo dhidi ya Liverpool kuwa ilikuwa muhimu wasifungwe hasa kwa vile wanakabiliwa na mechi ngumu zijazo dhidi ya Fenerbahce Alhamisi jioni , Chelsea na Manchester City.
Rooney, ambaye kwa sasa akiwa na Man United amechezea mechi 4 akitokea benchi, amesisitiza kuwa yeye yupo tayari wakati wowote akiitwa kucheza.

0 comments:
Post a Comment