Hivi karibuni Ronaldo alimwagana na Miss Spain wa zamani Desire Cordero, na inaokena ameamua kuendelea na maisha yake ya mahusiano na mtu mwingine.
Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Ureno ameonekana akiwa kwenye mahaba mazito na mwanadada Georgina Rodriguez anayeishi pia katika jiji la Madrid.
Ronaldo alijaribu kuziuia asipigwe picha na mapaparazi lakini hakufanikiwa katika hilo baada ya picha zake kunaswa.
Cristiano aliamua kutupia kitu cha wig kichwani pamoja na capelo zinazovaliwa kwenye mchezo wa baseball pamoja na miwani ya jua (sunglasses) ikiwa ni mbinu za kujaribu kukwepa lens za camera lakini kwa namna picha zinavyoonesha ni kwamba jaribio lake lilifeli.
Jarida la Chi liliotea bonge la picha wakati Ronaldo aki-enjoy busu la mpenzi wake Georgina Rodriguez walipokuwa kwenye mtoko wao jijini Paris.

Tetesi zinaonesha namna ambavyo Ronaldo aliweza kukutana na kifaa hicho kupitia mitandao ya kijamii.
Fununu zilizopo zinaeleza kwamba, wawili hao walikutana kwenye event ya D&G huku ikielezwa Ronaldo kuanza kumpeleka Santiago Bernabeu siku za hivi karibuni.
Baadhi ya picha kutoka kwenye account ya Instagram ya mlimbwende Georgina Rodriguez






0 comments:
Post a Comment