Posts za wanasoka mbalimbali baada ya ajali ya ndege ya wachezaji wa Brazil

Jamii ya wapendasoka ulimwenguni kote wameonekana kuguswa na ajali ya ndege iliyohusisha timu ya  Chapecoense ambayo imetokea usiku wa kuamkia leo.

Ndege hiyo iliyoanguka njiani ilikuwa imebeba klabu hiyo ya nchini Brazil kuelekea Colombia kwaajili mchezo wao mkondo wa kwanza wa michuano ya Copa Sudamericana  dhidi Atletico Nacional.
 
Timu hiyo ilikuwa icheze kunako dimba la Estadio Atanasio Girardot huko Medellin kesho Jumatano lakini ndege yao iliyokuwa ina abiria takriban 72 ilianguka njiani ikiwa Medellin wakati inatoka Santa Cruz de la Sierra huko Bolivia, na kubakisha watu watano tu wakiwa salama.
 
Mamlaka mbalimbali zimeripoti kuwa maafisa wa ndege hiyo walitangaza hali ya hatari majira ya 22.00 kwa saa za huko baada ya kukumbwa na matatizo ya kiufundi.
 
Ndege hiyio inasadikiwa kuanguka maeneo ya Cerro Gordo huko manispaa ya La Union
Wanandinga mbalimbali katika ulimwengu wa soka wameamua kutumia akaunti zao za mitandao ya kijamii kutoa pole kutokana na janga hilo la Chapecoense.
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment