WAZIRI NAPE ALIVYOSISITIZA USHIRIKIANO WA VYOMBO VYA HABARI TANZANIA NA CHINA NA FAIDA ZAKE


Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amesema ushirikiano wa karibu kati ya vyombo vya habari vya Tanzania na vile vya China, vinaweza kuongeza ufanisi katika fani ya habari.

Waziri Nape aliyasema hayo wakati wa uzinduzi wa hafla ya uzinduzi wa kongamano la waandishi wa habari ambalo lilihudhuriwa na waandishi kutoka Tanzania na China wapatao 30.


"Wachina sisi ni ndugu zetu, kama ushirikiano kati yao na sisi utadumishwa. Utasaidia ukuaji wa haraka wa tasnia ya habari.

"Tunaweza kualikana kwa ajili ya mafunzo na mambo mbalimbali kwa nia njema," alisema.

Katika mkutano huo, Naibu Waziri wa Chama cha Ukomunisti, Sun Zhijun pia alihudhuria na kuhamasisha suala hilo la ushirikiano na mafunzo.


Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment